Psalms 8:1-4
Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Daudi)
1 aEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Umeuweka utukufu wako
juu ya mbingu.
2 bMidomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao
umeamuru sifa,
kwa sababu ya watesi wako,
kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.
3 cNikiziangalia mbingu zako,
kazi ya vidole vyako,
mwezi na nyota,
ulizoziratibisha,
4 dmwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,
binadamu ni nani hata unamjali?
Copyright information for
SwhKC