Psalms 8:1-4

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Daudi)


1 aEe Bwana, Bwana wetu,
tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako
juu ya mbingu.

2 bMidomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao
umeamuru sifa,
kwa sababu ya watesi wako,
kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.


3 cNikiziangalia mbingu zako,
kazi ya vidole vyako,
mwezi na nyota,
ulizoziratibisha,

4 dmwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,
binadamu ni nani hata unamjali?
Copyright information for SwhKC